Вход на сайт

Просмотр новости

Найдите то, что Вас интересует

Kevin Keegan afariki dunia, chanzo chatajwa

Дата публикации: 20-07-2026 15:11:59

Keegan amefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu ugonjwa wa saratani ya tumbo, ambao Machi mwaka huu ulibainika kuwa umefikia hatua ya nne.

Основное содержимое страницы с новостью.

By  Mwandishi Wetu

Mwananchi Digital

Mwananchi

Muktasari:
  • Baada ya kustaafu kucheza, Keegan alijikita kwenye ukocha, akizinoa Newcastle United, Fulham, timu ya taifa ya England na Manchester City.

London, England. Nyota wa zamani wa Liverpool, Newcastle United na timu ya taifa ya England, Kevin Keegan, amefariki dunia leo Jumatatu, Julai 20, 2026 akiwa na umri wa miaka 75.

Keegan amefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu ugonjwa wa saratani ya tumbo, ambao Machi mwaka huu ulibainika kuwa umefikia hatua ya nne.

Taarifa iliyotolewa na familia yake imesema kifo cha Keegan kimeacha pengo kubwa, huku ikieleza kuwa nyakati zake za mwisho alikuwa amezungukwa na mke wake pamoja na watoto wake.

“Ni kwa huzuni kubwa sana tunatangaza kwamba Kevin Keegan amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 75.

“Aliyekuwa mchezaji na kocha wa timu ya taifa ya England alikuwa akipambana na ugonjwa wa saratani, na katika dakika zake za mwisho alikuwa amezungukwa na mke wake pamoja na binti zake.

“Kevin, mshindi wa tuzo ya Ballon d'Or mara mbili, alikuwa mume, baba na babu aliyependwa sana. Familia inapenda kuwashukuru madaktari na timu yote ya wataalamu wa afya waliomhudumia Kevin kwa msaada wao mkubwa,” ilisema taarifa hiyo.

Familia yake imeomba faragha katika kipindi hiki kigumu.

Keegan, ambaye ni miongoni mwa wachezaji waliowahi kupata mafanikio makubwa katika soka la England, alichezea klabu sita tofauti na kufunga mabao 204 katika michezo 592.

Kati ya klabu hizo, Liverpool na Newcastle United ndizo zilizompa umaarufu mkubwa, huku pia akiichezea England mara 63.

Akiwa Liverpool, Keegan alishinda mataji mbalimbali ikiwemo Ligi ya England na Kombe la Ulaya kabla ya kuhamia Hamburg ya Ujerumani, ambako aliendelea kung'ara na kutwaa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Ulaya (Ballon d'Or) mara mbili.

Baada ya kustaafu kucheza, Keegan alijikita kwenye ukocha, akizinoa Newcastle United, Fulham, timu ya taifa ya England na Manchester City.

Newcastle United imesema imesikitishwa na kifo cha Keegan, ikimtaja kuwa mmoja wa watu waliokuwa na ushawishi mkubwa katika historia ya klabu hiyo.

“Kevin alikuwa zaidi ya mchezaji na kocha wa hadhi ya kipekee. Alikuwa moyo uliokuwa ukiipa uhai Newcastle United kwa vizazi vingi vya mashabiki.

“Akiwa mchezaji, alionyesha kipaji cha kiwango cha dunia, ari ya mafanikio na imani katika Uwanja wa St James’ Park. Akiwa kocha, aliamsha upya matumaini ya jiji letu na kuwapa mashabiki fahari,” ilisema klabu hiyo.

Keegan ataendelea kukumbukwa kama mmoja wa mastaa wakubwa wa soka la England, akiwa na historia ya mafanikio ndani na nje ya uwanja.

Схожие новости

#Наименование новостиТональностьИнформативностьДата публикации
1Lutto nel mondo del calcio: è morto un due volte Pallone d'Oro-5520-07-2026
2Хоккеист "Эдмонтона" Колби Кейв введен в медикаментозную кому0007-04-2020
3Хоккеист "Эдмонтона" Колби Кейв умер в возрасте 25 лет0011-04-2020
4Хоккеист "Филадельфии" Линдблом вылечился от рака0002-07-2020
5Умер легендарный английский футболист, обладатель двух «Золотых мячей»-10520-07-2026
6Канте покинул сбор "Челси" по состоянию здоровья0021-07-2019
7Умер чемпион Паралимпийских игр легкоатлет Евгений Кегелев0007-03-2020
8Чемпион Bellator завершил карьеру из-за болезни головного мозга0010-02-2020
9TikTok star Patriotic Kenny dead at 84: Navy veteran who campaigned for servicemen passes after cancer battle-2519-05-2026

Классификация: Спорт. Схожих патентов: 0. Схожих новостей: 9. Тональность: -5. Информативность: 5. Источник: www.mwananchi.co.tz.