Вход на сайт

Просмотр новости

Найдите то, что Вас интересует

Wakulima waonywa kutumia mbegu zilizothibitishwa

Дата публикации: 28-08-2026 17:26:15

Wakulima wa mahindi nchini wametahadharishwa dhidi ya kutumia mbegu zisizothibitishwa ubora huku wakihimizwa kuhakikisha wanahakiki mbegu kabla ya kupanda ili kulinda uwekezaji wao na kuongeza nafasi ya kupata mavuno bora.

Основное содержимое страницы с новостью.

Morogoro. Wakulima wa mahindi nchini wametahadharishwa dhidi ya kutumia mbegu zisizothibitishwa ubora huku wakihimizwa kuhakikisha wanahakiki mbegu kabla ya kupanda ili kulinda uwekezaji wao na kuongeza nafasi ya kupata mavuno bora.

Tahadhari hiyo imetolewa leo Jumamosi, Agosti 28, 2026 na Mkurugenzi wa Kampuni ya uzalishaji wa mbegu na viuatilifu ya Bayer Tanzania, Sango Mwinyi, mkoani Morogoro wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya “DEKALB Mafanikio Shambani."

Kampeni hiyo inalenga kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa kutumia mbegu halisi na suluhisho bora za kilimo.

Mwinyi amesema mabadiliko ya hali ya tabianchi yameendelea kuleta changamoto kubwa kwa wakulima wadogo, hali inayofanya upatikanaji wa mbegu zilizothibitishwa kuwa muhimu zaidi kuliko wakati mwingine wowote.

Amesisitiza uamuzi wa kununua mbegu bila kuzihakiki unaweza kusababisha wakulima kupanda mbegu zisizo sahihi na hatimaye kupata mavuno duni.

Kwa mujibu wake, taarifa sahihi na uhakiki kabla ya kupanda ni hatua muhimu katika kujihakikishia tija shambani.

Kampeni hiyo inalenga kuwahamasisha wakulima kutumia aina tano za mbegu chotara za mahindi za DEKALB, ambazo zimebuniwa kuendana na mazingira mbalimbali ya kilimo nchini, ikiwemo maeneo yenye mvua chache.

Mbegu hizo, kwa mujibu wa kampuni hiyo, zinalenga kuwasaidia wakulima kuongeza uzalishaji na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi ambazo zimekuwa zikiathiri sekta ya kilimo.

Mbali na ujumbe wa kulinda uwekezaji wa mkulima, kampeni hiyo pia inakuja na promosheni yenye zawadi mbalimbali, zikiwemo simu janja, pikipiki, pampu za kunyunyizia, mashine za kupandia na kumenya mahindi. Mwisho wa kampeni hiyo, wakulima wawili wanatarajiwa kujishindia Toyota pick-up kila mmoja, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha ushiriki na matumizi ya mbegu bora.

Mkulima wa mkoani Kilosa, Morogoro, Juma Abdallah amesema kutumia mbegu zisizo sahihi zinaweza kukufanya ukapoteza nguvu na fedha kwa kuwa unapata mavuno kidogo.

Схожие новости

#Наименование новостиТональностьИнформативностьДата публикации
1Madiwani waitaka halmashauri ya wilaya Mufindi  kulipa madeni05.0228-08-2026
2Govt Seeks Urgent Measures On Cement Prices06.8720-08-2026
3Warioba aeleza wasiwasi wake kupatikana Katiba mpya 202902028-08-2026
4Производители выступили против предложенных Минсельхозом соглашений по ценам на удобрения0017-03-2021
5Для КМНС предлагают ввести квоты на вылов рыбы для ведения хозяйственной деятельности0010-12-2021
6Россия с 15 марта вводит экспортные пошлины на кукурузу и ячмень0014-03-2021
7FPOs want to be treated like farmers, not corporates to get govt’s benefits07.3517-07-2026
8На Кубани предлагают предоставлять субсидии научным сельхозучреждениям наравне с аграриями0030-11-2021
9Аграриям уступили место в вагоне0529-04-2026
10В Казахстане предложили ввести запрет на ввоз зерна автомобильным транспортом0027-07-2022

Классификация: . Схожих патентов: 0. Схожих новостей: 10. Тональность: 0. Информативность: 6.87. Источник: www.mwananchi.co.tz.