Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa, wameitaka halmashauri hiyo kuweka mikakati ya kuhakikisha madeni ya walimu na watumishi wa kada nyingine yanalipwa kwa wakati, ili kuwawezesha kufanya kazi kwa utulivu na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma.
Ijumaa, Agosti 28, 2026

Baadhi ya madiwani waliohudhuria baraza hilo wakisikiliza baada ya kuwasilisha taarifa ya hesabu za mwisho za halmashauri kwa mwaka wa fedha 2025-2026.
Mufindi. Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa, wameitaka halmashauri hiyo kuweka mikakati ya kuhakikisha madeni ya walimu na watumishi wa kada nyingine yanalipwa kwa wakati, ili kuwawezesha kufanya kazi kwa utulivu na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma.
Ushauri huo umetolewa leo Ijumaa, Agosti 28, 2026 na Diwani wa Mpanga Tazara, Flaviana Mpanda na Diwani wa Mtwango, Monte Kilamlaya, baada ya kuwasilishwa kwa taarifa ya hesabu za mwisho za halmashauri kwa mwaka wa fedha 2025/26.
Taarifa hiyo iliwasilishwa katika kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi.
Kilamlaya amesema halmashauri inapaswa kutafuta namna bora ya kulipa madeni hayo kwa wakati, ili kupunguza changamoto za kiuchumi zinazowakabili watumishi na kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kwa utulivu.
Amesema baadhi ya watumishi wamekuwa wakikabiliwa na changamoto za kifamilia na kiuchumi kutokana na madeni hayo, hali inayoweza kuathiri utendaji wao kazini.
“Halmashauri yetu hii ni kubwa, basi tuonyeshe ukubwa wetu. Tuhakikishe madeni haya yanalipwa kwa wakati ili walimu wawe na utulivu wakati wa kufundisha wanafunzi, kwani mwisho wa siku tunakuwa na matokeo mabaya. Vitu vingine tunasababisha sisi wenyewe kama halmashauri,” amesema.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Castory Masangula amesema amepokea ushauri wa madiwani na kwamba baraza limeelekeza madeni ya watumishi wa kada mbalimbali, wakiwemo walimu, yalipwe.
Amesema kulipa madeni hayo kutasaidia watumishi kufanya kazi katika mazingira bora na kwa ari zaidi.
“Baraza limeshauri tulipe madeni haya ili watumishi hawa waweze kufanya kazi katika hali ya furaha, kwa sababu kama uchumi wako hauko vizuri huwezi kufanya kazi vizuri,” amesema Masangula.
Awali, akiwasilisha taarifa hiyo, Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani, Fredrick Kibwana, amesema hadi kufikia Juni 30, 2026, halmashauri ilikuwa na madeni yenye thamani ya Sh1.6 bilioni.
Amesema madeni hayo hayahusiani na mishahara, bali yanajumuisha madai ya walimu ya Sh535 milioni, watumishi wasio walimu Sh488 milioni, wazabuni Sh629 milioni na Bohari Kuu ya Dawa (MSD) Sh21 milioni.
Katika hatua nyingine, Mwenyekiti Masangula amesema Baraza la Madiwani limeishauri halmashauri kuhakikisha fedha zinazotengwa kwa ajili ya Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (Tarura), zinatumika katika kutengeneza barabara za kimkakati.
Amesema hatua hiyo inalenga kuwawezesha wananchi kusafirisha mazao yao kabla ya kuanza kwa msimu wa mvua unaotarajiwa mwezi Oktoba.
Amesema halmashauri inakusanya ushuru kupitia barabara hizo, hivyo ni muhimu fedha zinazotengwa kwa ajili ya matengenezo zielekezwe kwenye maeneo yenye umuhimu mkubwa kiuchumi.
“Sisi kama halmashauri tunakusanya ushuru kupitia barabara hizi, hivyo kupitia fedha ambazo tunazitenga za asilimia 10 tunawapa Tarura ili kutengeneza barabara zetu za kimkakati, wananchi waweze kupitisha mazao yao mbalimbali kwenye barabara hizo,” amesema Masangula.
| # | Наименование новости | Тональность | Информативность | Дата публикации |
|---|---|---|---|---|
| 1 | Wakulima waonywa kutumia mbegu zilizothibitishwa | 0 | 6.87 | 28-08-2026 |
| 2 | KCMC yaitaka NIMR kuharakisha ‘One-Stop Centre’ | 0 | 8.96 | 28-08-2026 |
| 3 | Watenegenezaji, waingizaji dawa feki za asili kusakwa, NIMR kufungua kiwanda | 0 | 7.71 | 28-08-2026 |
| 4 | Kilio cha abiria Stendi ya Magufuli chaanza kutatuliwa | 0 | 10 | 28-08-2026 |
| 5 | Минобрнауки предложило заключать договоры целевого обучения со студентами для АЗРФ | 0 | 0 | 09-06-2021 |
| 6 | В Магаданской области запустили ежегодную акцию «Собери ребенка в школу» | 0 | 9.27 | 27-07-2026 |
| 7 | Минпросвещения планирует привлечь студентов к работе в школьных кружках | 0 | 0 | 16-08-2019 |
| 8 | Магаданский промышленный техникум начал приемную кампанию для абитуриентов | 0 | 8.01 | 11-06-2026 |
| 9 | Мишустин поручил повысить качество практикоориентированности программ в вузах | 0 | 0 | 19-05-2025 |