Вход на сайт

Просмотр новости

Найдите то, что Вас интересует

Bunge kumthibitisha Ndejembi leo

Дата публикации: 28-08-2026 05:50:08

Soma hapa...

Основное содержимое страницы с новостью.

Dodoma. Bunge la Tanzania leo Ijumaa, Agosti 28, 2026 litapokea na kumthibitisha uteuzi wa Deogratius Ndejembi kuwa Makamu wa Rais.

Kwa mujibu wa orodha za shughuli za Bunge leo, pamoja na mambo mengine, wabunge watapata fursa hiyo kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania.

 Jumatano ya Agosti 27, 2026, Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ilimpendekeza Ndejembi ambaye ni Waziri wa Nishati kuwa Makamu wa Rais.

Ndejembi ambaye pia ni Mbunge wa Chamwino, Mkoa wa Dodoma anakwenda kuchukua nafasi ya Dk Emmanuel Nchimbi ambaye ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo.

Baada ya Bunge kudhibitisha, itabaki kuapishwa na kuanza majukumu mapya ya kumsaidia Rais Samia Suluhu Hassan.

Kwa mujibu wa taarifa ya Bunge, Ndejembi alianza elimu ya msingi Cannon Andrea kuanzia mwaka 1988–1995, kisha akasoma sekondari ya Kigurunyembe mwaka 1996–1998 na Merton College 2002–2004.

Kati ya mwaka 2006–2009 alisoma Shahada ya International Relations katika University of Lincoln nchini Uingereza. Baadaye, mwaka 2009–2012, alisoma Advanced Diploma katika Institute of Administrative Management.

Kabla ya kuwa mbunge, Ndejembi aliwahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Dodoma. Mwaka 2020, alipitishwa na CCM kuwa mgombea wa ubunge wa Jimbo la Chamwino.

Amewahi kuhudumu unaibu Waziri Ofisi ya Rais, (Utumishi wa Umma na Utawala Bora) kabla ya kuingia kwenye nafasi ya uwaziri kamili. 

Julai 2024, Rais Samia alimteua Ndejembi kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Kabla ya kushika Umakamu wa Rais Ndejembi alikuwa Waziri wa Nishati.

Схожие новости

#Наименование новостиТональностьИнформативностьДата публикации
1Ndejembi awakuna wadau, apewa angalizo01027-08-2026
2Hivi ndivyo Dk Nchimbi anavyoweza kurudi CCM01027-08-2026
3Kinachofuata kwa Dk Nchimbi01027-08-2026
4UWT: Hakuna mwanachama aliye juu ya CCM01028-08-2026
5Jaji Warioba afichua alichozungumza na Dk Nchimbi kabla, baada ya kujiuzulu01027-08-2026
6Utata ukomo umakamu wa rais wa Nchimbi, wanasheria watofautiana08.427-08-2026
7Migogoro inapogeuka rafiki wa ndoa01009-08-2026
8Ijue siri ya kisukari iliyojificha kwenye wali, ugali01007-08-2026
9Zacharia: Mhitimu la saba anayetamba kwenye uhandisi01025-08-2026
10UCHAMBUZI WA MJEMA: Tusijidanganye, tunahitaji maandalizi haya kabla ya 2030018.3327-08-2026

Классификация: Информация. Схожих патентов: 0. Схожих новостей: 10. Тональность: 0. Информативность: 10. Источник: www.mwananchi.co.tz.